Ubatizo, Ushiriki Mtakatifu

Mwandishi: 
Jari Rankinen
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Mchungaji anamwaga maji juu ya kichwa cha mtoto na kumbatiza yeye katika jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Na kama hili halikufanyika kwa mtoto, linaweza kufanyika hata kwa mtu mzima. Kwa nini?

Yesu aliamuru tupatize. Alisema kwamba kupitia ubatizo mtu hufanyika kuwa mwanafunzi wake. Kupitia ubatizo tunakuwa watoto wa Mungu, na kupata zawadi ya msamaha wa dhambi na uzima wa milele. Biblia inasema tulivikwa Kristo wakati wa ubatizo. Kutoka hapo kuendelea mbele kimbilio letu ni ndani ya kile Yesu anafanya kwa ajili yetu.

Ni asili yetu kushangaa ni kwa jinsi gani maji yanaweza kufanya mambo makubwa kama haya. Mungu ameahidi kutenda wakati mtu anabatizwa. Ameahidi kumchukua mtu kama mtoto wake,kumsamehe na kumwokoa. Mungu amechagua njia hii kutufanya sisi wake kwa kile Yesu alifanya. Hakika kuna hekima kubwa kwa kazi Mungu aliyofanya kwa njia ya Yesu Kristo.

"Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkawabatize kwa jina la Baba, na Mwana na Roho mtakatifu”.
(Mathayo 28:19-20, SUV)

Mwandishi: 
Jari Rankinen
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Nilibatizwa zamani. Hii ina maana gani sasa? Je ina maana yeyote? Kwa mimi ubatizo una maana kubwa wakati nikiwa mtoto nilibatizwa sikuwa na la kufanya sikujua, wala kufanikiwa au kubadilisha. Si hata kitu kidogo. Nikiwa ndani ya kutokamilika, kutokujua au kuwa mzuri- nilifaa kwa Mungu. Nilikuwa mkamilifu kwa sababu Yesu alikufa kwa ajili yangu na aliyepatanisha dhambi zangu. Ilikuwa hivyo na iko hivyo sasa. Hivi ndiyo ubatizo unavyonikumbusha mimi.

Tunaweza kujikumbusha kila asubuhi maana ya ubatizo wetu una maana gani: kama nilivyo mimi ni mali ya Mungu na ninaenda mbinguni. kama nilivyo, ninawezakupata suluhisho kwa Yesu. Sasa hii inaleta furaha na heshima. Hili ni jambo ambalo linaleta nguvu na kuishi kama mkristo na kuishi kwa mapenzi ya Mungu hata kama kwa kiasi kidogo.

Biblia hufundisha kwamba tumeokolewa kwa neema. Kwa kuokolewa kwa neema ina maana kwamba tunaweza kuwa mali ya Mungu pasipo kuwa na kuchangia na kuipata mbingu kama jinsi tulivyo na yote hii ni kwa sababu ya kazi ya Yesu msalabani. Kila mtu aliyebatizwa na kuamini katika Yesu ataokolewa kwa neema.

“Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu."
(Efeso 2:8 SAV)

Mwandishi: 
Jari Rankinen
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Biblia inasema kwamba ili uokolewe unahitaji ubatizo na imani. Lazima tuwe macho ni nini Mungu alisema kuhusu hilo. Vinginevyo tutakuwa hatarini kuachwa nje ya kazi yake ya ukombozi. Kwa hiyo lazima tuwabatize watoto wetu na kupokea ubatizo sisi wenyewe kama bado hatujabatizwa.

Biblia inasema kwamba baadhi ya watu waliookolewa pasipo kubatizwa. Katika ijumaa kuu, Yesu alisema kwa yule mwaalifu aliyekuwa karibu yake kwamba atakuwa pamoja naye paradiso. Huyu mtu alikuwa hajabaptizwa. Mungu anaweza fanya kazi hata nje ya vyombo vya neema ambavyo ametuambia kuvitumia. Anaweza kuokoa hata bila ubatizo. Lakini mtazamo huu wa kiuungu hauturuhusu sisi, kudharau ubatizo ambao ametuamuru sisi tuupokee. Kama wakristo tumefungwa katika mafundisho ya Agano jipya: Katika ubatizo tunafanyika kuwa wakristo na watoto wa Mungu. Wakati mtoto aambaye hajabatizwa akifa tunaweza kusema tu kwamba yeye yuko mikononi mwa Mungu wetu mwenye Rehema.

“Aaminiye na kubatizwa ataokoka, asiyeamini atahukumiwa.”
(Marko 16:16 SUV)

Mwandishi: 
Jari Rankinen
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Wewe unayependa mambo ya imani na hujabatizwa unaweza shangaa kama utatakiwa kubatizwa. Naam unahitaji. Wasiliana na mchungaji au mfanyakazi wa usharika wa kanisa la Kilutheri. Pamoja na mchungaji mnaweza kwenda moja kwa moja katika mafungu muhimu ya imani na baadaye unaweza kubatizwa,au ungelipenda kubatizwa lakini si rahisi labda uko chini ya umri wa mika 15 au wazazi wako hawapendi wewe ubatizwe. Unaweza kumwanini Yesu ijapokuwa hujabatizwa. Omba ubatizwe mara tu kama ulivyoamua.

Labda una mtoto mdogo ambaye hajabatizwa? Inafaa mtoto huyu abatizwe? Ndiyo. Wasiliana na mchungaji au mfanyakazi wa usharika na mpange ubatizo.

“Petro akawaambia, tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpaate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapoke kipawa cha Roho mtakatifu kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu walio mbali na kwa wote watakaitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”
(Matendo ya mitume 2:38-39 SUV).

Mwandishi: 
Jari Rankinen
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Biblia inafundisha kwamba ubatizo hauitaji kurudiwa. Unatolewa thamani hubaki hivyo daima. Hii haibadiliki hata kama tunamkataa Mungu baada ya ubatizo wetu. Tunaweza wakati wote kumrudia Baba yetu anatusubiri sisi.

Hata hivyo kuna wale wanaotaka kubatizwa tena au wameshabatizwa tena. Na kuna wale wanaobatiza watu tena. Wengi wao wanaweza kufikiri kwamba kama mtu akibatizwa akiwa mtoto si ubatizo halisi. Haya ni madai hatari. Hii inamaana kwamba hujabatizwa na wewe si Mkristo. Wengine wanasema kama mtu wakati wa ubatizo hakuelewa mara moja maana ya kubatizwa kwamba huo sio ubatiso halisi. Lakini ubatizo ni tendo la Mungu ambalo halitengemei ni kiasi gani mtu anaelewa. Hatukuelwa ni nini kilitokea wakati Yesu alikufa juu ya msalaba kwa ajili- hatukuepo wakati lilitokea lakini lilikuwa ni tendo la Mungu na wokovu wetu.

Hivyo basi ubatizo hautakiwi kurudiwa, mtu anayepokea ubatizo mara ya pili anafanya kosa. Yetote ambaye amekosa anatakiwa kutubu kwa Mungu na kuomba msamaha. Na Mungu anasamehe wote wanaotubu kwa sababu Yesu alizipatanisha dhambi za watu wote.

“Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.“
(Efeso 4:5 SUV)

Mwandishi: 
Jari Rankinen
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Wakristo wanashiriki meza ya Bwana (Ekarisiti) kama Yesu alivyoamuru. Kila wakati wote wanaposhirikishwa, maneno ya Yesu yanayofanya Ushirika mtakatifu yanasomwa. Meneno yake yamechukuliwa kutoka katika maandiko matakatifu ya Biblia ambayo yanasemwa nini kilitokea Yerusalemu usiku kabla ya kifo cha Bwana Yesu. Yesu na wanafunzi wake walisherehekea sakramenti ya meza ya Bwana, na Yesu aliwaambia waendelee kufanya hivyo baadaye.

Katika maneno ya Meza ya Bwana yanasema kwamba mkate ambao tunaumega ni mwili wa Bwana Yesu na mvinyo ni agano jipya katika damu yake. Katika ya Mathayo, Yesu alisema pia ni damu yake. Vivyo hivi mwili na damu vipo katika meza ya Bwana inashirikishwa. Ina maana kwamba Yesu yupo ndani ya mkate na mvinyo kwa njia maalum. Tunakutana naye naye anakutana na sisi. Unapofikiri utakuwa karibu na Yesu, nenda shiriki katika meza ya Bwana. Huu ni muujiza mkubwa wa meza ya Bwana. Yesu yuko pale na anafanya kazi ndani yetu.

Katika ushirika mtakatifu mara nyingi unaweza usihisi kana kwamba untakutana na Yesu. Lakini mawazo yetu hayawezi kumzuia Yesu kuja karibu yetu. Yeye yupo pale alipoahidi kuwa na haijalishi tunafikiri. Aliahidi kuwa katika meza ya Bwana-Mkate ni mwili wake, ana mvinyo ni damu yake.

"Nao walipokuwa wakila Yesu alitwaa Mkate, akabariki, akaumega, akawapa wanafunzi wake, akasema, Twaeni mle; huu ndio mwili wangu. Akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, Nyweni nyote katika hiki, kwa maana hii ndio damu yangu ya agano, imwagikayokwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi."
(Mathayo 26:26-28, SUV)

Mwandishi: 
Jari Rankinen
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Katika ushirika mtakatifu tunakutana na Yesu, na hili ni nzuri kwetu kwa njia nyingi. Mkombozi wetu ana utume: Anasamehe. Hivi ndivyo Yesu anafanya katika ushirika mtakatifu. Anashirikisha kile alichopata katka mauti yake. Kifo chake kilipatanisha dhambi za watu wote na kuleta msamaha kwa wingi kama watu watakavyohitaji.

Dkt. Martin Luther aliijua Biblia kwa uzuri sana. Kwa swali ”Kuna nini kizuri katika Ushirika Mtakatifu” anajibu: “katika sakaramenti hii dhambi zetu zote zinasamehewa” tunapata uzima na baraka, kwa maana penye msamaha wa dhambi kuna pia uzima na baraka.”

Kila anayeamini yale Biblia imeahidi anakuja katika ushirika mtakatifu na kupokea mwili na damu ya Yesu kwa ondoleo la dhambi. Biblia imeahidi kwamba katika ushirika matakatifu Yesu anatoa msamaha wa dhambi. Hii inaweza kuonekana tu nyepeso na rahisi . Lakini huruma za Mungu ni rahisi. Ila Mara nyingi tunazifanya tu kwa ngumu.

“Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele na nitamfufua siku aya mwisho.”
(Yohana 6:54 SUV)

Mwandishi: 
Jari Rankinen
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Ushirika mtakatifu ni kwa wakristo waliokwisha kubatizwa. Katika Kanisa la Kilutheri wale wote waliokwisha kwenda katika kipaimara na wameshabarikiwa wanaweza kupokea ushirika mtakatifu. Hivi ndivto inaweza kuhakikishwa kuwa washirika wameelewa maana ya ushirika mtakatifu na kujua tofauti ya ushirika mtakatifu na kula na kinywaji cha kawaida. Pia watoto waliofundishwa wanaweza kupokea meza ya Bwana pamoja na wazazi au wazee wao. Na kila mmoja anaweza kuja madhabahuni kubarikiwa.

Wakati mwingine unaweza kujihisi vigumu kwenda kwa meza ya Bwana. Mwingine anweza kujisikia kwamba wema wake hautoshi kupekea sakramenti, kwamba lazima awe mwenye imani imara. Hivyo ndivyo inavyotakiwa iwe. Meza ya Bwana si kwa ajili ya uzuri wetu tulionao au kwa wale waliofanikiwa kaika maisha. Kinyume chale meza ya Bwana ni kwa wale wote wanohitaji msamaha wa dhambi. Katika ushirika mtakatifu rafiki na mkombozi ana rehema kwa wale wote walioshindwa. Ushirika mtakatifu ni kwa wale wote wanaohitaji msamaha wa dhambi. Meza ya Bwana si kwa wale wote wanofikiri kuwa hawamwitaji Yesu Kristo.

Biblia inatuonya sisi juu ya kwamba mtu anaweza kula na kunywa mwili na damu ya Yesu kwa hukumu yake mwenyewe. Baadhi ya watu ambao onyo hili lilipewa, kwa asili ni wale ambao kupokea meza ya Bwana na hawakufikiri kwamba ni ushirika mtakatifu. Walikula na kunywa hata kulewa . na mkate na mvinyo viliweza kuliwa bila utaratibu. Paulo aliandika kwamba ambaye anapokea ushirika mtakatifu na hajui ni mwili wa Kristo, atakuwa anakula na kunywa hukumu yake mwenyewe. Onyo hili mara nyingi limeeleweka vibaya, na kukataa ushirika mtakatifu kwa wale wote ambao si wema, na imani zao ni dhaifu. Lakini hii si maana yake.

“Maana kila mlapo mkate huu na kukinywea kikombe hiki, mwaitangaza mauti ya Bwana hata ajapo.”
(1 Korintho 11:26 SUV)