Imani na wokovu

Mwandishi: 
Pasi Palmu
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Siku moja tajiri mmoja alimuuliza Yesu nitawezaje kuurithi uzima wa milele. Huyo mtu aliishi maisha mazuri. Yesu alimwambia auze mali yake yote na kuwapa maskini hizo fedha kisha amfuate Yesu. Tajiri alihuzunika sanakwa sababu aliulizwa zaidi. Wanafunzi walichanganyikiwa na kuanza kumuuliza Yesu ”Mtu anawezaje kuokolewa?” Yesu aliwajibu, kwa wanadamu hilo haliwezekani bali kwa Mungu yote yanawezekana.

Ili ni jibu la Kikristo.

Tumefungwa na ubinafsi wetu wenyewe, tunajipenda wenyewe kuliko kuwapenda wenzetu. Nguvu zetu za kupata wokovu ni za kibinafsi pia. Je unalo tumaini lolote?

Jibu ambalo Ukristo unatupa ni to tofauti na dini zingine. Mtazamo wetu si juu ya yale mwanadamu atafanya. Yesu Kristo ndiye kiini cha kila kitu. Yesu alifanya kile ambacho sisi tusingeweza kufanya. Alichukua mashtaka yetu mbele za Mungu na kupatanisha dhambi zetu na maovu yetu msalabani.

Hii ndio maana kunayo msamaha kalimifu katika moyo wa Mungu. Umetangazwa kwetu katika Biblia. Inaitwa injili ”Habri njema”. Na tunaridhi hiyo kwa imani. Kwa imani katika Yesu Kristo tunaokolewa na kuweza kuingia mbinguni. Nilipobatizwa katika jina la Mungu Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu na ninatambua kwamba mimi ni mali ya Mungu. Siku ya hukumu sitajaribu kujibu juu ya mashtaka ya dhambi zangu kwa Yesu amelipa deni langu la dhambi zangu zote.

Tunaweza kuwa na hakika kuhusu kuingia mbinguni maana unaweza kuwa na uhakika juu kazi ya Yesu.

Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani;ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu."
(Efeso 2:8-9, SUV)

Ombi: Yesu nizaidie nipate kukuamini.
Mwandishi: 
Ville Auvinen
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Imani iokoayo siyo kazi ya mwanadamu bali ni zawadi itokayo kwa Mungu. Mwanadamu hawezi kwa asili kuzalisha imani yeye mwenyewe au kuamua kuja katika imani. Kwa jumla inategmea Mungu. Msingi wa kwanza wa vyombo vya neema ni neno la Mungu. Katika ubatizo imani inazalishwa kupitia neno pamoja na maji. Katika chakula cha meza ya Bwana imani iliyounganika na mkate na mvinyo. Na katika ungamo la dhambi inaunganishwa na msamaha wa dhambi.

Roho mtakatifu anazungumza na mwanadamu kupitia neno la Mungu. Na kupitia neno hilo Roho mtakatifu anakuja ndani ya roho ya mwanadamu na kuzalisha imani. kuamsha na kuimarisha imani ni kazi muhimu za Roho Mtakatifu.

Kama unashangaa labda una imani au hauna ya kutosha unaweza kumuomba Mungu akuimarishie imani. Hili ni ombi ambalo Mungu analojibu kulingana na hitaji. Unaweza kuamini kwamba Mungu anakupa imani lija ya au unavyojihishi au unavyojizoesha.

Katika kanisa Roho anamtukuza Yesu Kristo kama Mwokozi na kuhakikisha kwamba neema inakutosheleza pia. Imani siyo kitu chetu tunachokisukuma au kujaribu ila ni kazi ya Mungu ndani ya mtu.

"Basi imani, Chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo."
(Rum 10:17, SUV)

Mwandishi: 
Sirkka-Liisa Huhtinen
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Muumini ni msharika katika Kanisa. Wakristo wanaunganishwa na wakristo wengine; kusikiliza neno la Mungu, kuomba, na kushiriki meza ya Bwana tena uunganishwa kwa kusudi maalumu. Yote haya yanaimarisha, na kulinda imani. Roho Mtakatifu yupo kutuimarisha sisi.

Amri za Mungu zinatuhusu sisi sote. Kama mkristo hatuwezi kuzidharau Amri za Mungu na mapenzi ya Mungu baba yetu wa mbinguni.

Kila mmoja wetu hapa ana wito wake, na Mungu anataka tuwe waaminifu katika kuhudumia watu wanao tuzunguka. Hata hivyo wakati tunapokumbana na mahitaji ya maisha haya, mara moja tunatambua kuwa mwisho wetu kama binadamu na kwamba nguvu zetu hazitoshi. Tujisikia wadhaifu. Na hivyo tunajaribu kufanya kile kilicho kinyume na Amri za Mungu na dhambi.

Asili ya ubinadamu wetu, mwili wakati wote unatuingiza katika dhambi na kufanya yale yaliyo kinyume na mapenzi ya Mungu haijalishi wewe ni mkristo au la! Hivyo tunahitaji msamaha wa Mungu usio na kikomo, kuomba na nguvu zitokazo kwa neno la Mungu.

Maisha katika imani hata hivyo si kukana vitu na kujitahidi kuwa bora. Kama Mkristo tunaishi kama watoto wa Mungu ndani ya uhuru na usalama ndani ya Neema yake. Katika Kristo Yesu tunapewa imani, tumaini na upendo kama zawadi. Hii ndiyo sababu Mkristo anapenda kusogea karibu na Yesu.

"Kama vile Baba alivyonipenda mimi, nami nilivyowapenda ninyi, kaeni katika pendo langu."
(Yoh 15:9, SUV)

Ombi: Bwana Mungu nisogeze karibu na Yesu katika njia zako. Usiniaje nipoteze njia yangu.
Mwandishi: 
Ville Auvinen
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Uhakika wa wokovu hauwezi kutegemea kazi yeyote ya mwanadamu, hisia na, matendo yake kwa sababu siku zote siyo kamili na zinaweza anayebadilika kila wakati. Usalama unaweza tu kutegemea kazi ya Mungu na ahadi zake.

Kwanza, Biblia inasema Mungu aliupenda ulimwengu na alifanya upatanisho na pamoja nasi kwa kusulubishwa kwa Kristo. Kwa hiyo Yesu alikuja kwa ajili yako pia.

Pili, kama umebatizwa umeunganishwa na kazi ya wuokovu ya Kristo. Hivyo wewe ni sehemu ya wokovu ambao ni ya ulimwengu wote.

Tatu, Biblia inafundisha kwamba atakaye amini na kubatizwa ataokoka.

Sehemu si katika nguvu za imani ila ni malengo yake: Kristo na ahadi za Mungu. Wakati sisi wenye imani havivu tunapomgeukia na kuomba msaada kutoka kwa Yesu hii inaitwa imani. Yesu anasamehe dhambi kwa sababu Biblia inaahidi “Yeyote atakayeliitia jina la Bwana ataokoka”. Imani pia zawadi kutoka kwa Mungu; Si uwezo na kazi ya mwanadamu mwenyewe. Hivyo basi kama umebatizwa na kurudi kwa Yesu na kuomba msamaha wa dhambi zako na kuomba wokovu, upo katika njia ya kwenda mbinguni.
Kwa kushiriki chakula cha Bwana na ahadi za Mungu ambazo umeunganishwa nayo kukupa nguvu na kuimarisha imani yako.

“Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho. kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu,nami hukaa ndani yake”.
(Yoh 6:54-56, SUV)

Mwandishi: 
Liisa Rossi
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Dini zingine hujibu swali jinsi ya kuishi maisha mema na kumkaribia Mungu. Ukristo hutoa jibu tofauti. Mtazamo si kwetu ila yale Mungu amefanya.

Dini zingine hukuongoza utakavyo mtii Mungu, kutenda mema au kujaribu uwezavyo ili uweze kubarikiwa na uweze kufikia wokovu. Ukristo una ujumbe tofauti: Kila kitu kilifanyika tayari kwa Baraka na wokovu. Hatuwezi kujikokoa ila Yesu alituondelea dhambi. Tumeokolewa kwa neema, kwa kupokea zawadi tuliyopewa na Mungu. Hatuhitaji kufanya chochote ili kufanya Mungu atupende. Anatupenda kabisa. Tunaweza kutulia katika imani katika Mungu na kuwatumikia wengine na upendo ambao Mungu anatupa.

Msingi wa Ukristo ni neema ya Mungu. Ni neema tu katika Kristo ambayo itatuokoa. Dini zote ambazo zimejengwa juu ya uwezo wako na matendo huelekea upotevuni na kukata tama.

Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
(Yohana 14:6, SUV)

Bwana, ninataka kukuamini lakini mimi ni mnyonge na nina mashaka. Nizaidie!
Mwandishi: 
Pasi Palmu
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Ndio wapo. Uumbaji wa Mungu kwa hakika hauzuiliwi na huu ulimwengu unaonekana kama kiburi cha mwanadamu kinavyofikiriwa, hatuwezi kuthibiti uumbaji wa Mungu. Ulimwengu wa Mungu ni mwingi zaidi ya mengi rangi na za kushangaza zaidi ya sisi na zaidi ya sayansi yetu inavyoweza kuchunguza.

Malaika hapana hata hivyo katika mtazamo wa Ukristo wakati unasoma injili utaona kwamba malaika waliunganishwa katika matukio muhimu ndani ya maisha ya Yesu. Pia wanaitwa “Roho ziokoazo” hivyo hutimiza kazi ya uenezi ambao Mungu aliwapa wao hapa duniani juu ya yote walihudumu katika kusudio la kuokoa Roho.

“Hao wote si roho watumikao wakitumwa kuhudumia wale watakaorithi wokovu?"
(Waebrania 1:14, SUV)