Bahati mbaya au Mungu

Mwandishi: 
Liisa Rossi
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Mojawapo ya mahitaji muhimu ya mwanadamu ni kutafuta maana ya maisha. Tunaweza kutafuta maana ya maisha kwa kutenda mema, katika watu ambao tunawapenda, kazini, katika kuendeleza maisha, katika kutafuta hekima na mengine mengi, ila katika mambo haya yote hakuna hata moja ambalo linaweza kutosheresha kabisa swali la kina lililo katika mioyo yetu.

Sehemu ya kuanzia kutafuta maana kamili ya maisha ni kutambua kuwa tumeumbwa ili katika maisha tuwe na uhusisiano na Mungu. Kadiri tunavyoishi mbali na Mungu, jambo la maana linalokosekana katika maisha yetu. Jambo la maana na muhimu ni kuishi katika maana tuliumbwa kwayo, maanake kuishi katika uwepo wa Mungu, bila dhambi au uovu ambao unaweza kututenganisha naye. Hivyo jambo muhimu katika maisha yetu ni kumfahamu Yesu, ambaye ndiye maisha ya kweli. Kwa imani katika yeye tutafika nyumbani kwa baba yetu wa mbinguni.

Hata kama hatima ya maisha yetu ya mwisho ya maisha yetu ni mbinguni, maisha yetu hapa duniani si kwamba ni bure na hayana maana. Tuna nafasi ya pekee katika kupendwa na Mungu, kumpenda and kutangaza upendo wake miongoni mwetu.

nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu.
(Wafilipi 3:14, SUV)

Mungu, wakati sijui au sielewi, nionyeshe njia ya kuendea.
Mwandishi: 
Liisa Rossi
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Fikiria juu ya compyuta au simu ambayo unatumia kusoma ujumbe huu. Je unaweza kumwamini mtu akikwambia kwamba chombo hicho kiko kama kilivyo kwa bahati wakati sehemu muhimu za hiyo simu zilikutana tu kwa bahati mbaya? Hata hivyo unajua mara moja kwamba mtu amepanga na kukitengeneza chombo hicho kwa sababu maalum? Dunia kunamoishi ndani yake je? Ni mtindo wa ajabu na wa kina sana kuliko chombo chochote kilichjotengenezwa. Mwili wa mwanadamu ni kitu cha ajabu ambacho unaweza kusitajabia. Kitu cha namna hii kisinge weza kuepo kwa bahati mbaya.

Kwa upande mwingine, dunia inaweza kuwa na machafuko, kugongana na hali ya mabariko. Hata hivyo, kuna Muumbaji wa ajabu nyuma ya kila jambo– na Baba mpendwa ambaye anajitambulisha kupitia Kristo. Dunia yote na kila mmoja wetu huishi kwa uwezo wa Munug. Aliumba dunia na kupangilia kila kitu kuwa viende sawa sawa. Hakuna kitu ambacho kiko kwa bahati tu, ila kwa kusudi kamili. Hakuna maisha ya mtu yeyote ambayo ni kwa bahati. Unaishi kwa sababau Mungu alikupanga uwepo. Misha yako yametokana na kusudi na mpangilio kamili na upendo mkuu.

Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.
Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita.
(Mwanzo 1:1, 26-27, 31).

Mungu, fungua macho yangu ili nione vipaji vyako. Fungua midomo yangu ili nikushukuru na moyo wangu ukusifu.
Mwandishi: 
Liisa Rossi
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Watu wengi hufikiri kwamba kwa njia fulani kuna Mungu, yaani nguvu na uwezo wa juu. Kuna anayeweka hufahamu juu ya mema na mabaya katika watu. Kuna anayeongoza hatima ya historia kwa mkono wake. Hata mtu asiyeamini Mungu ana sheria fulani “Mungu” ambaye anategemea na ambaye anayemwona kuwa mwenye mamalaka fulani.

Hisia tu na maoni au hakikisho juu ya uwepo wa Mungu haitwambii chochote kuwa Mungu ni nani , anaonekanaje, na jinsi tunaweza kumfahamu. Ujumbe kamili kuhusu Mungu unatoka kwake tu, neno lake katika Biblia. Mungu ni mkuu na amefichika na hatuwezi kufahamu kwa mawazo ya kibinadamu ambayo yana upungufu kwa sababu ya dhambi. Hii ndio sababu tunahitaji kuamini tangazo lake. Mungu aliuumba dunia na anaiongoza na kuitawala. Na zaidi sana–Mungu alifanyika mwanadamu katika Kristo Yesu hapa duniani na akatuondoa kutoka dhambi zetu. Hakuna mwingine na wala hakuna Mungu mwingine.

Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.
(Ufunuo 1:8)

Mungu, ninaamini kwamba wewe si wa kutumainia tu na kuogovya. Unisikie na kunijibu.
Mwandishi: 
Liisa Rossi
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Tunapoona ubaya na mateso yapo kwetu-pengine hata katika maisha yetu-inawezekana tukauliza wazo juu ya Mungu na mwenye enzi na Mungu mwenye upendo. Hata hapo tunaweza kugeukia neno la Mungu ambalo linaweza kutegemewa kuliko mawazo yetu ambayo yana upungufu.

Kulingana na Biblia Mungu ni Bwana wa mabwana na mfalame wa wafalme ambaye anatawala dunia nzima. Anaona na anajua kila kitu na hakuna chochote kinaweza kutendeka bila yeye kuruhusu. Kutokana na anguko la mwandamu, Shetani amepewa uwezo duniani. Hata hivyo nguvu zake haziwezi, wala kufika popote bila Mungu kuruhusu. Shetani tayari amepoteza maana an nafasi dhidi ya nguvu ya Mungu. Yesu alishinda nguvu za dhambi kupitia kwa kifo chake msalabani na kufufuka kwake.

Mara kwa mara ni vigumu kwetu kuelewa nia za Mungu, hata hivyo tunaweza kumwamini kuwa yeye nidye anaye ongoza yote. Mungu mwenye enzi anaona kikamilifu, Anajua yaliyo mema kwa ajili yetu. Mungu aliukmba ulimwemungu kwa nene la kinywa chake, na anaweza kuitunza. Na dunia yote inaweza kuona ukuu wa Mungu.

”Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, BWANA, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.”
(Isaya 40:28)

Bwana, una nguvu zote. Naomba nipate kinga na matumaini katika nguvu zako.
Mwandishi: 
Ville Auvinen
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Kwa usahihi kabisa mtu hawezi kumtafuta Mungu,lakini Mungu ndiye anayemtafuta na kumpata mwanadamu. Mungu anaishi mahali pa juu sana mahali ambapo mwanadamu hawezi kufika, lakini yeye amekuja na kufanya kuwa karibu na sisi na kututafuta. Mungu amejifunua peke yake katika sakramenti, neno lake (Biblia) katika ubatizo na ushirika mtakatifu pia katika maungamo ya dhambi na masamaha ya dhambi. Katika hayo inatupasa kumtafuta huko.

Kama umebatizwa inakupasa kujikumbusha mwenyewe maana yake. Katika ukiri wa imani ya mitume na kateksimo ni mahali pazuri pa kuanzia kujifunza hata kama hujabatizwa ni vizuri kuanzia hapo. Na pia nakutia moyo kusoma Biblia, anza kusoma agano jipya na hasa INJILI.

Tafuta kanisa unaweza kuhiriki katika ibada ya jumapili. Kipindi cha ibada unaweza pamoja na ushirika kukiri na kuungama na kupokea tangazo la msamaha wa dhambi na kusikia mafundisho kutoka katika biblia. Kwa ushirika meza ya Bwana tunakuwa karibu na Mungu. Mungu anakutana nasi katika mkate na katika mvinyo- mkate ukiwa ni mwili wa Kristo na mvinyo ukiwa ni damu ya Kristo.

“Nami nitawatafuta waliopotea, nitawarudisha waliofukuzwa, nitawafunga waliovunjika nitawatia nguvu wagonjwa nao wanono na wenye nguvu nitawaharibu nitawalisha hukumu."
(Ezekieli 34:16, SUV)

Ombi: - Bwana Mungu ninataka nikukutafuta na kukujua wewe, nizaidie nipate njia kwako