Biblia ni nini?

Mwandishi: 
Erkki Koskenniemi
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Biblia ni kitabu muhimu cha Ukristo. Kulingana na imani yetu, Mungu anatuzungmzia katika Biblia, anatwambia sisi ni nani, nafasi yetu ni ipi mbele za Mungu, nafasi yetu katika dunia ya Mungu na Mungu anatarajia nini kutoka kwetu.

Agano la kale na Agano Jipya, sehemu zote mbili zina uhusiano wa karibu, na zimetolewa kwetu na Mungu kupitia watu. Hutengeneza Biblia nzima: Inaanza na kuumbwa kwa binadamu, ikifuatwa na anguko lake na jinsi Mungu aliandaa njia ya kumrejesha kwa kumtoa mwanae kwetu. Biblia inaanza na uumbaji na umaliza nayo− Kutakuwa na hukumu ya mwisho, dunia tunamoishi sasa itapotea, Mungu ataumba dunia mpya mahali atapeleka wote wamwaminio Kristo.

Bibilia nzima imeandikwa na watu lakini wakati huohuo tunaamini Biblia nzima ni neon la Mungu. Mungu ametupa neno lake katika hali ambayo iko katika hali ya unyonge kwa njia nyingi- Angeandika ujumbe wake kwa moto au atume malaika wake walitangaze. Lakini ilikuwa katika unyonge pia wakati mtoto alipowekwa katika hori la ngombe katika Bethrehemu. Hii ndiyo inaonekana kuwa njia Mungu anayofanya kazi. Japo si njema kwa wenye hekima na matajiri, ni hazina ya wanyonge na masikini.

Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.
(Zaburi 119:105)